Askofu Roger Abasha ambaye anaongoza ujumbe wa Kanisa la Orthodox la Canada katika mji wa Quds huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu, amesema kuwa mauaji ya umati yanayofanywa dhidi ya wananchi wasiokuwa na hatia wa Palestina katika Ukanda wa Gaza katika kipindi hiki cha kukaribia mwaka mpya wa Miladia ni kitendo cha kuumiza na kusikitisha.
Askofu Mkuu wa Canada amelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kusimamisha haraka iwezekanavyo ukatili na vitendo visivyokuwa vya kibinadamu vinavyofanywa na Israel dhidi ya raia wa Ukanda wa Gaza. 339574