IQNA

Papa aitaka Iran kutatua mgogoro wa Gaza

12:15 - January 18, 2009
Habari ID: 1732408
Papa Benedict wa XVI wa Kanisa Katoliki Duniani ameitaka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kufanya juhudi za kumaliza mgogoro wa Ukanda wa Gaza ambao umeanzishwa na uchokozi wa utawala haramu wa Israel na kujaribu kurejesha amani na utulivu katika ukanda huo.
Kiongozi wa Wakatoliki ametoa witi huo alipokutana na ujumbe wa maaskofu wa kanisa hilo wa Kiirani huko Vatican, ambapo amesisitiza kwamba Iran inapasa kutumia nguvu yake kubwa katika kujaribu kumaliza mgogoro huo na hatimaye kurejesha amani na utulivu katika Mashariki ya Kati.
Papa Benedict amesema kuwa Kanisa Katoliki linaunga mkono mtu au kundi lolote lile linalofanya juhudi za kuimarisha amani na utulivu ulimwenguni. Amesema, Iran ni daraja la kuziunganisha nchi za Mashariki ya Kati na za Asia na kwamba kwa yakini inaweza kuwa na nafasi muhimu katika kurejesha amani katika eneo hilo nyeti.
Kiongozi huyo wa Wakatoliki duniani amewataka Wakatoliki nchini Iran kushirikiana na serikali na kuwataka maaskofu wa Iran kuwashawishi wafuasi wao waendelee kubaki nchini kwao ili washirikiana na serikali katika kustawisha nchi yao na kuiletea maendeleo ya kuridhisha.
Wafuasi wa Kanisa Katoliki nchini Iran wanapata 25,000. 349687
captcha