IQNA

Warsha ya mafunzo ya "Taswira ya Uislamu Katika Nchi za Magharibi"

9:29 - January 20, 2009
Habari ID: 1733306
Warsha ya mafunzo kuhusu Taswira ya Uislamu Katika Nchi za Magharibi inafanyika Sana'a Yemen kwa shabaha ya kutayarisha uwanja wa mazungumzo kwa wanafunzi wa leo na viongozi wa kesho.
Warsha hiyo ambayo ni sehemu ya mpango wa mazungumzo ya kiutamaduni kati ya Ujerumani na Yemen, imetayarishwa na ubalozi wa Ujerumani mjini Sana'a, Chuo Kikuu cha Sana'a na Chuo Kikuu Huria cha Berlin.
Warsha hiyo inayowashirikisha wanafunzi na wahadhiri wa vyuo vikuu vya Yemen na Ujerumani inachunguza mtazamo wa Magharibi kuhusu ulimwengu wa Kiislamu na maisha ya Waislamu.
Malengo mengine ya warsha hiyo ni kuondoa mtazamo mbaya kuhusu dini ya Kiislamu, kuimarisha uhusiano kati ya Waarabu na nchi za Magharibi, kuchunguza matukio ya Ukanda wa Gaza na kushirikiana katika kuzuia matukio mengine kama hayo. 350647
captcha