Kwa mujibu wa tovuti ya Leadership Nigeria, chuo kikuu hicho ambacho kimejengwa pambizoni mwa msikiti wa An'yas katika mji wa Kano, kinafungamana na chuo kikuu cha Bairo na kitakuwa chini ya usimamizi wa Wizara ya Elimu ya Nigeria.
Chuo hicho kitakuwa cha kwanza cha elimu ya juu cha Qur'ani katika eneo la magharibi mwa Afrika.
Waislamu ambao ndio wengi kati ya wakazi wa kaskazini mwa Nigeria wanaunda asilimia 55 ya jamii nzima ya nchi hiyo. 354928