IQNA

Kitabu cha 'Uislamu na Sanaa ya Zama' chachapishwa nchini Libya

12:02 - February 19, 2009
Habari ID: 1745836
Kitabu cha 'Uislamu na Sanaa ya Zama' kimechapishwa na kusambazwa kwa lugha ya Kihispania nchini Libya kwa udhamini wa Taasisi ya Wito wa Kiislamu ya nchi hiyo AMAI.
Tovuti ya taasisi hiyo imesema kuwa, kitabu hicho kinaakisi mifano ya sanaa ya kisasa ya Kiislamu ambayo imetumika katika pembe mbalimbali za dunia. Kitabu hicho kinachambua kwa urefu sanaa hiyo.
Kitabu hicho vilevile kina maelezo kuhusiana na athari ya sanaa hiyo ya Kiislamu katika nchi zisizo za Kiislamu na hasa za Magharibi. 365816
captcha