IQNA

Warsha ya kumuarifisha Mtume Muhammad (saw) huko Buenos Aires

9:09 - February 23, 2009
Habari ID: 1747422
Kituo cha Kiislamu cha Buenos Aires kinachofungamana na Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislamu nchini Argentina kimeandaa warsha ya kuarifisha na kumtambulisha Mtume Muhammad (saw) kwa watu wa nchi hiyo.
Waandaji wa warsha hiyo wanasema kuwa lengo lake hasa ni kutafuta njia bora zaidi za kumuarifisha Mtume Muhammad (saw) kwa watu wasiokuwa Waislamu na pia kuandaa uwanja wa kumfahamu zaidi mtukufu huyo.
Zaidi ya wahubiri wa Kiislamu, maimamu wa misikiti na wasimamizi wa vituo vya Kiislamu vya Argentina wapatao 50 wameshiriki katika warsha hiyo.
Ubalozi wa Saudi Arabia mjini Buenos Aires ndio ulioandaa warsha hiyo. 367639
captcha