Mkutano huo umeitishwa na jumuiya ya wanachuo Waislamu waliohitimu masomo katika vyuo vikuu vya Uingereza.
Mkutano huo utabuni na kuchunguza sera za mwaka ujao za Jumuiya ya Kiislamu ya Wanafunzi wa Vyuo Vikuu vya Uingereza na kueneza utamaduni wa Kiislamu na Kiirani kati ya wanachama wake na familia zao.
Mkutano huo pia utajadili jinsi ya kutekeleza maagizo ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei ya kuzidisha maarifa ya Kiislamu kwa wanafunzi wa kigeni wa vyuo vikuu hapa nchini. 368417