IQNA

Mkutano wa kwanza wa kimataifa wa 'Bustan ya Qur'ani' nchini Qatar

11:11 - March 01, 2009
Habari ID: 1749650
Taasisi ya Malezi, Sayansi na Ustawi wa Kijamii ya Qatar imeandaa mkutano wa kwanza wa kimataifa wa 'Bustani ya Qur'ani' ambao umeanza leo Jumapili katika hoteli ya As-Sharq nchini humo.
Maonyesho hayo yatakayoendelea kwa muda wa siku tatu yanawashirikisha wataalamu 20 wa mimea iliyotajwa na Qur'ani pamoja na maudhui tofauti za bustani na shamba katika Qur'ani. Wataalamu hao ni kutoka nchi kama vile Malaysia, Pakistan, Misri, Palestina, Morocco, nchi wanachama wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi, Marekani, Malaysia na Indonesia.
Halima Bint Ali, Waziri wa Elimu ya Juu wa Malaysia ni miongoni mwa watu waliopangiwa kuzungumza katika mkutano huo.
Mimea katika Qur'ani, hadithi za Mtume (saw) na elimu mpya, mazingira na kuhifadhiwa kwake katika mtazamo wa Kiislamu, sanaa ya Kiislamu, uchoraji na maendeleo pamoja na usanifu majengo wa Kiislamu ni miongoni mwa mambo yatakayojadiliwa katika mkutano huo. 370111
captcha