IQNA

Kikao cha Japan na ulimwengu wa Kiislamu chafanyika nchini Kuwait

13:58 - March 12, 2009
Habari ID: 1755183
Kikao cha mazungumzo ya tamaduni mbili za Japan na ulimwengu wa Kiislamu kilianza Jumatano katika hoteli ya Sheraton nchini Kuwait.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Kuwait KUNA, kikao hicho cha siku mbili kinachochunguza matunda ya fikra za Kiislamu kimeandaliwa na Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Kuwait na kwa usimamizi wa Nawaf Ahmad al-Jabir Swabah, Mriti wa Kiti cha Ufalme wa nchi hiyo.
Washiriki wa kikao hicho watachunguza njia za kuimarisha mazungumzo kati ya Japan na ulimwengu wa Kiislamu katika mitazamo mbalimbali.
Kikao hicho kilichoanza saa tatu kimehudhuriwa na Hussein Nassir al-Hureiti, Waziri wa Wakfu na Masuala ya Kiislamu wa Kuwait. 376529
captcha