Msomaji wa Qur'ani raia wa Tanzania aliyeshiriki katika mashindano ya kimataifa ya Qur'ani na hadithi yaliyoandaliwa hivi karibuni na Jamuiya ya Kimataifa ya al-Mustafa (saw) amesisitiza kwamba mashindano ya kimataifa ya Qur'ani yanayoandaliwa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yamepelekea Wasuni na wananchi wa nchi nyinginezo duniani kubadili msimamo na mtazamo wao kuhusiana na Iran na Waislamu wa madhehebu ya Shia.
Hayo yamesemwa na Khamis Swadiq, msomaji Qur'ani wa Tanzania anayeshiriki katika duru ya 14 ya mashindano ya kimataifa ya Qur'ani na hadithi hapa nchini Tehran.
Amesema, amekuwa akijishughulisha na usomaji Qur'ani kwa kipindi cha miaka mitatu sasa ambapo anawaiga wasomaji wa Kiirani katika uwanja huo.
Amesema, watu wengi wamekuwa wakipotoshwa na dhana mbovu zinazoenezwa na maadui wa Uislamu kwamba, Mashia wana Qur'ani tofauti lakini kwamba wametambua jambo hilo kuwa ni upotofu mkubwa baada ya kuitembelea Iran na kuona kwamba ina wasomaji wazuri sana wa kitabu hicho kitakatifu.
Khamis Swadiq amesema hatua ya Iran ya kuandaa mashindano mbalimbali ya Qur'ani ni jambo ambalo limeimarisha nafasi ya Waislamu wa Kishia duniani. 377884