Habari zinasema kuwa lengo la kuasisiwa kituo hicho ni kushiriki katika masuala ya elimu na uhakiki wa kisayansi wa kimataifa kuhusu dini ya Kiislamu na kuimarisha mijadala ya kimantiki kuhusu kadhia hiyo.
Kituo cha ISISI ni nakala iliyofanyiwa marekebisho ya kituo cha ISIM kilichoasisiwa mwaka 1998 katika mji wa Leyden nchini Uholanzi.
Kituo cha ISISI kitachunguza pia ustawi wa masuala ya kijamii, kisiasa na kiutamaduni cha jamii za kisasa za Kiislamu.
Vyuo vikuu vinne vya Uholanzi vitashirikiana na kituo hicho katika masuala ya utafiti wa Kiislamu.
Gharama za kuendesha kituo hicho kwa kipindi cha miaka mitatu ya awali zitatolewa na Chuo Kikuu cha Leyden. 380822