IQNA

Kongamano la Uislamu na Pluralism linafanyika leo Sri Lanka

13:50 - March 29, 2009
Habari ID: 1758688
Kongamano la Uislamu na Pluralism (mfumo unaotambua mawazo, misimamo na dini mbalimbali) linafanyika leo katika mji wa Colombo nchini Sri Lanka.
Mkutano huo unaosimamiwa na Baraza la Kueneza Amani la Sri Lanka, unahudhuriwa na wawakilishi wa nchi za kigeni, viongozi wa kidini na kisiasa na wawakilishi wa jumuiya za kimataifa.
Mwanafikra wa Kiislamu wa Sri Lanka Dakta Shukri na Maulawi Abdullah Mahmoud, Mwenyekiti wa Baraza la Maulamaa wa Kiislamu ni miongoni mwa watu wanaohutubia mkutano huo. 381000

captcha