IQNA

Mashindano ya taifa ya Qur'ani yaanza Imarati

0:53 - April 12, 2009
Habari ID: 1763335
Mashindano ya kumi ya taifa ya kuhifadhi Qur'ani Tukufu yameanza leo nchini Imarati yakisimamiwa na Idara ya Masuala ya Kiislamu ya Dubai.
Mashindano hayo yanawashirikisha wanaume na wanawake kutoka vituo vya Qur'ani ya Umoja wa Falme za Kiarabu na yataendelea kwa kipindi cha wiki moja.
Hamad Muhammad Abdurrahman ambaye ni miongoni mwa maafisa wanaosimamia mashindano hayo amesema kuwa washindani 210 ambao 120 kati yao ni wanawake wnachuana katika mashindnao hayo.
Washiriki wanashindana kuhifadhi Qur'ani nzima, juzuu 20, juzuu 10 na juzuu 5. 385957

captcha