IQNA

Jihad ya siri; nembo nyingine ya kuendelea chuki dhidi ya Uislamu nchini Marekani

13:59 - April 13, 2009
Habari ID: 1764137
Jarida la kila wiki la Human Events linalochapishwa nchini Marekani limechukua hatua nyingine ya kiburi ya kusambaza kitabu kiitwacho Jihadi ya Siri miongoni mwa wasomaji wake na hivyo kuendeleza chuki na uadui dhidi ya Uislamu nchini humo.
Kitabu hicho ambacho anwani yake kamili ni, Jihadi ya Siri; Jinsi Uislamu Wenye Itikadi Kali Marekani Unavyotoweka Bila Kutumiwa Mabomu, kilichoandikwa na Mmarekani Robert Spencer kimekuwa kikisambazwa bure na jarida la Human Events miongoni mwa wasomaji wake. Katika kitabu chake hicho kilicho dhidi ya Uislamu Spencer anadai kwamba Uislamu unaenezwa nchini Marekani na makundi ya jihadi kwa lengo la kuitokomeza nchi hiyo kwa njia isiyo ya moja kwa moja na bila ya kutumiwa mabomu.
Robert Spencer ni miongoni mwa Wakristo wenye misimamo mikali na ya chuki dhidi ya Uislamu nchini Marekani ambaye hadi sasa ameandika vitabu vingi vinavyolenga kudhalilisha na kuutusi Uislamu na Mtume Muhammad (saw).
Baadhi ya vitabu vya mwandishi huyo mwenye chuki dhidi ya Uislamu ni pamoja na Uhakika wa Muhammad, Muasisi wa Dini Yenye Taasubi Kubwa Zaidi Duniani na Ukweli Kuhusu Muhammad; Muasisi wa Dini Yenye Itikadi Kali Zaidi Duniani.
Gazeti la Marekani la Human Events pia mwaka uliopita lilisambaza bure vitabu hivyo vya matusi dhidi ya Uislamu miongoni mwa wasomaji wake. 386761
captcha