IQNA

Kuanza masomo ya teolojia na sheria za Kiislamu nchini Zimbabwe

22:50 - April 16, 2009
Habari ID: 1765739
Masomo ya muda ya teolojia na sheria za Kiislamu kwa ajili ya wanawake yameanza kutolewa nchini Zimbabwe chini ya usimamizi wa Kitengo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Harare.
Wanawake wa Kiislamu wanaoshiriki katika mafunzo hayo wanajifunza sheria za fiqhi na misingi ya itikadi za Kiislamu.
Kitengo cha Utamaduni cha Iran nchini Zimbabwe pia kinapanga kutayarisha masomo ya muda ya sheria na itikadi za Kiislamu katika mji wa Kadoma. Shughuli nyingine za kitengo hicho ni pamoja na kuitisha mkutano wa kuchunguza matatizo ya wanawake na mkutano wa kukumbuka siku ya kufariki dunia hayati mam Khomeini. 38842
captcha