IQNA

Kikao cha uchumi wa Kiislamu nchini Malaysia

16:24 - April 19, 2009
Habari ID: 1766958
Kikao cha kimataifa cha Uchumi wa Kiislamu na Uchumi wa Umoja wa Nchi za Kiislamu kitafanyika mjini Kuala Lumpur nchini Malaysia tarehe 28 na 29 za mwezi huu wa Aprili.
Kwa mujibu wa tovuti ya Tradechakra, kikao hicho kimeandaliwa na Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Malaysia na Benki ya Ustawi wa Kiislamu kwa lengo la kuimarisha uchumi wa Kiislamu. Uchumi wa Kiislamu, masuala ya benki za Kiislamu, uchumi wa nchi za Kiislamu wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu OIC, ushirikiano wa kiuchumi miongoni mwa nchi wanachama wa OIC na mafunzo kuhusiana na masuala ya kifedha na uchumi wa Kiislamu ni miongoni mwa masuala yaliyopangwa kujadiliwa katika kikao hicho. 390085
captcha