Mwandishi wa IQNA nchini Afghanistan ameripoti kuwa Rais Hamid Karzai wa nchi hiyo ametuma salamu za rambirambi kwa taifa la nchi hiyo akisisitiza kwamba atautaka uongozi wa vikosi vya askari wa kigeni nchini humo kutoa maelezo kuhusua mauaji hayo.
Rais Karzai amesema amesikitishwa mno na mauaji hayo na akazitaka Wizara za Ulinzi, Mambo ya Ndani na taasisi husika kuchunguza tukio hilo na kuwafuatilia wahusika. Amesema kuwa kuuawa kwa mwanazuoni huyo mkubwa ni hasara kubwa kwa jamii ya Afghanistan.
Sheikh Maulawi Abdulqahir alikuwa miongoni mwa maulamaa wakubwa wa Afghanistan katika mkoa wa Logar. Aliuawa Jumamosi iliyopita akiwa nyumbani kwake katika shambulizi la ndege za kivita za nchi za Magharibi. 391048