Akizungumzia suala hilo, Sheikhatu as-Salman mkuu wa kituo hicho amesema kuwa, ratiba ya kikao hicho cha siku mbili itajumuisha masuala mbalibali zikiwemo hotuba zinazohusu masuala ya Qur'ani, mashindano ya burudani, futuhi na tamthiliya, filamu za kweli, maonyesho ya vitabu vya kidini na kasida. Amesema kikao hicho kimeandaliwa kwa ajili ya kuwafahamisha wasichana na wanawake burudani salama za Kiislamu, kugundua vipawa vya washiriki, kutumia vizuri nafasi za wasichana na wanawake katika familia na kuimarisha moyo wao wa kuhisi kuwa na majukumu katika jamii. 392944