IQNA

Kikao cha 'Mafunzo ya Qur'ani' kufanyika nchini Ufaransa

8:03 - May 05, 2009
Habari ID: 1773989
Kikao cha Mafunzo ya Qur'ani, kimeandaliwa kufanyika tarehe 10 Mei na taasisi ya Utafiti wa Kiislamu ya Mediterranean IMEM huko katika mji wa Strasbourg nchini Ufaransa.
Kwa mujibu wa Saphirnews, washiriki wa kikao hicho watachunguza tafsiri ya Qur'ani na misingi yake, kuhakiki maudhui mbalimbali kuhusiana na historia ya kuteremka aya za Qur'ani na lugha ya kitabu hicho cha wayhi wa Mwenyezi Mungu.
Abdel Hakim Boussande, mtaalamu wa lugha ya Kiarabu na mhadhiri katika Kituo cha Kiislamu cha Chateau Chinon, atatoa mafunzo ya lugha hiyo kwa washiriki wa kikao hicho ambao hatimaye watapewa vyeti maalumu na vyenye itibari. 399384
captcha