Mashindano ya Qur'ani kwa wanawake wa Imarati ambayo yamefanyika chini ya anwani ya Zawadi ya Hamida bint Muhammad bin Khalifa yalianza siku ya Ijumaa huko katika Kituo cha Kidini na Utamaduni cha Muhammad bin Khalid Aal Nahyan katika mji wa Abu Dhabi, ambao ni mji mkuu wa Umoja wa Falme za Kiarabu. Wanawake 57 wa Imarati waliohifadhi Qur'ani wanashiriki katika mashindano hayo.
Wanawake 57 wa Imarati waliohifadhi Qur'ani wanashiriki katika mashindano hayo. Shuma bint Khalid Aal Nahyan ambaye anasimamia mashindano hayo amesema kuwa malengo ya kufanyika mashindano hayo ni kuwashajiisha wanawake wa Imarati waliohifadhi Qur'ani kuisoma kwa mbinu ya tajweed, kuwashawishi wanawake zaidi wafanye juhudi za kuhifadhi Qur'ani na vilevile kuwapa moyo wa kushiriki katika mashindano mbalibali ya Qur'ani. Sherehe za kushukuriwa na kutunukiwa zawadi washindi wa mashindano hayo zitafanyika kesho Jumapili katika kituo kilichotajwa. 401661