IQNA

Duru za masomo ya Qur'ani Gilgit, Pakistan

17:02 - May 16, 2009
Habari ID: 1779037
Duru za masomo ya Qur'ani maalumu kwa vijana wa kike na kiume wa Pakistan zitaanza hivi karibuni katika eneo la milimani la Gilgit lililoko kaskazini mwa nchi hiyo.
Katika kipindi cha miaka mine iliyopita, duru kama hizo za masomo ya Qur'ani zimekuwa zikiendeshwa na walimu wenye uzoefu mkubwa katika usomaji wa Qur'ani ambao wanasimamiwa na Hujjatul Islam wal Muslimeen Dhakir Hussein Irfani, ambaye amehitimu masomo yake katika Kituo cha Kimataifa cha Mustafa (saw) mjini Qum. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, hivi sasa pia mwanafunzi mwingine wa kike aliyehitimu masomo yake katika Chuo Kikuu cha az-Zahra cha mjini Qum nchini Iran, kila siku hutoa mafundisho ya Qur'ani kwa wanafunzi wa kike na kiume katika eneo hilo la Gilgit. 405494
captcha