IQNA

Kuchunguzwa misingi ya kijamii ya Qur'ani nchini Uingereza

12:57 - May 17, 2009
Habari ID: 1779311
Duru za masomo za kuchunguza misingi ya kijamii ya Qur'ani Tukufu, zitakuwa zikifanyika kila siku ya Alkhamisi nchini Uingereza ambapo Ali Ramadhan Al-Ausi, mtafiti wa Qur'ani raia wa Iraq na muhadhiri katika Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Masomo ya Kiislamu mjini London katika Kituo cha Kiislamu cha Uingereza.
Katika duru hizo za uchunguzi, Ustadh al-Ausi atakuwa akijadili masuala mbalimbali kama vile ya uadilifu, rehema kuhusiana na watu dhaifu, kulea watoto wema na kuweka misingi mizuri kwa ajili ya kujenga jamii iliyosalimika. Mambo mengine yatakayojadiliwa katika duru hizo za uchunguzi ni pamoja na; mtazamo wa Qur'ani kuhusiana na wanadamu wote na kuwataka wamwogope Mwenyezi Mungu na kujiweka mbali na maasi na dhambi, kuwa na uhusiano mzuri na jamaa, uchunguzi wa riwaya za Mtume Muhamma (saw) na Maimamu Maasumu (as) kuhusiana na suala hilo na aya za Qur'ani zinazozungumzia uumbwaji wa mwanadamu. 405782
captcha