Kwa mujibu wa makubaliano yaliyofikiwa kati ya serikali ya Tatarstan na Idara ya Masuala ya Kidini ya Uturuki, m aimamu wa swala za jamaa wa misikiti ya Uturuki watatumwa kusalisha katika misikiti ya Tatarstan katika mwezi mkukufu wa Ramadhani.
Aidha maulamaa hao wa Uturuki watakuwa na jukumu la kutoa darsa za Qur'ani na mafunzo mengine ya Kiislamu katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Jamhuri ya Tatarstan iko katika Shirikisho la Russia lakini ina mamlaka ya kujiendeshea shughuli zake na aghalabu ya wakazi wake ni Waislamu.
627515