Kwa mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha Masuala ya Qur'ani katika Wizara ya Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu, Hujjatul Islam Hamid Mohammadi, maonyesho hayo yatafunguliwa baada ya sala za Magharibi na Ishaa.
Akizungumza na Shirika la Habari la Qur'ani IQNA, Hujjatul Islam Hamid Mohammadi ameongeza kuwa sherehe za ufunguzi zitahudhuriwa na Ayatullah Mahdavi Kani, Hujjatul Islam Sayyid Ahmad Alamulhuda na Waziri wa Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu Sayyed Muhammad Husseini. Sherehe hizo zitaanza kwa kiraa ya Qur'ani Tukufu itakayosomwa na Saeed Tusi.
Maonyesho ya 18 Kimataifa ya Qur'ani Tukufu yana washiriki kutoka nchi 25 duniani. Kaulimbiu ya maonyesho ya mwaka huu ni "Qur'ani, Kitabu cha Maisha".
Maonyesho hayo yataendelea hadi tarehe 23 ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.
627457