Nakala hiyo ya Qur'ani ya dhahabu yenye thamani kubwa imetayarishwa na taasisi ya Moscow Mint ya ilionyeshwa katika maonyesho ya mwaka jana ya kaligrafia mjini Moscow.
Qur'ani hiyo ya dhahabu imechapishwa kwa mujibu wa nakala ya hati za Othman Twaha inayotambuliwa kuwa ndiyo ya zamani zaidi ya kitabu cha Mwenyezi Mungu. Nakala hiyo ya Othman Twaha inahifadhiwa katika Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Mashariki ya Academia ya Sayansi Russia katika mji wa Saint Petersburg. Nakala hiyo ya Qur'ani yenye uzito wa kilo 14 imetengeneza na kiwanda cha kufua dhahabu cha Moscow kwa kipindi cha miezi 18.
Nakala hiyo ya Qur'ani imekwishaonyeshwa katika nchi za Bahrain, Misri, Libya na maonyesho ya kimataifa ya Qur'ani ya Tehran. 629475