Qur'ani hiyo ambayo ni ya kwanza ya aina yake ilianza kuandikwa na Muirani Ali Yazdaniyan kwa kutumia kompyuta mwaka mmoja uliopita.
Mwandishi wa mbinu hiyo ya Qur'ani amesema kuwa ameamua kufanya hivyo ili kunufaika na kitabu hicho kitakatifu ambayo ni neema kubwa ya Mwenyezi Mungu kwa mwanadamu na pia kusisitiza juu ya umoja wa umma wa Kiislamu ambayo ni amri muhimu ya Mwenyezi Mungu na mafundisho ya Mtume Wake Mtukufu (SAW).
Maandishi hayo ya Qur'ani yamewavutia watu wengi wanayoyatembelea maonyesho hayo ya Tehran ambayo yamepangwa kuendelea katika kipindi chote cha mwezi mtukufu wa Ramadhani. 631642