Kwa mujibu wa shirika rasmi la habari la Yemen, mashindano haya ya kila mwaka yamefanyika katika Ukumbi wa Taasisi ya Kitaifa na Kiutamaduni ya Vijana wa mji wa Ta'izz katika fremu ya shughuli za kila mwaka za Mwezi wa Ramadhani za taasisi hiyo.
Katika mashindano hayo washiriki 90 kutoka maeneo mbali mbali ya Yemen wameshriki katika mashindano ya viwango vya kuhifadhi Qurani kamili, kuhifadhi Juzuu 10 na Juzuu 20 za Qurani Tukufu.
Mashindano haya yanafanyika kwa mwaka wa saba mfululizo na waandalizi wanasema lengo ni kuihudumia Qurani Tukufu na kuimarisha uwezo wa wasichana na wanawake katika kuihifadhi Qurani Tukufu.
643205