Kwa mujibu wa gazeti la Zaman la Uturuki, hivi karibuni Sarrazin aliwashambulia vikali wahajiri wa Kiislamu na Waarabu katika kitabu chake alichokipa jina la 'Ujerumani Yajitokomeza Yenyewe' akiwatuhumu kuwa ni hatari kubwa kwa usalama wa nchi hiyo.
Vilevile kwa amri ya Rais Christian Wulff wa Ujerumani mwanasiasa huyo mbaguzi alifukuzwa kutoka kwenye Jopo la Idara ya Benki Kuu ya Ujerumani kutokana na matamshi yake hayo ya kibaguzi.
Sarrazin amefukuzwa katika chama cha SPD kutokana na wingi wa kura za wanachama waliokerwa na misimamo yake ya kibaguzi. 647921