IQNA

Mwanaharakati wa Kishia Saudi abuni taasisi ya kuunga mkono Qur'ani

17:51 - September 08, 2010
Habari ID: 1990599
Sayyed Hassan al Namr Mousawi ambaye ni kati ya wanaharakati wa Kishia huko Saudi Arabia amebuni Jumuiya ya Umma ya Kutetea Qur'ani kufuatia hatua ya kishenzi ya kanisa moja la Marekani ya kutangaza siku ya kuiteketeza moto Qur'ani.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, Sayyed Mousawi amesema lengo la kubuni jumuiya hiyo ni kuwaleta pamoja Waislamu na hata wasio kuwa Waislamu ili kukabiliana na kanisa hilo la Marekani ambalo limeamua kuyavunjia heshima matukufu ya Kiislamu.
Itakumbukwa kuwa kanisa moja lenye misimamo ya kufurutu mipaka la Marekani limetangaza kuwa tarehe 11 mwezi huu wa Septemba litaitekeleza kwa moto Qur'ani Tukufu, hatua ambayo inaendelea kulaaniwa kote duniani.
651159
captcha