IQNA

Saini milioni moja kupinga kuchomwa moto Qurani Marekani

7:56 - September 14, 2010
Habari ID: 1993202
Wanaharaakti wa intaneti wamepanga kukusanya saini milioni moja kupinga hatua ya kishenzi ya kuchoma Qurani Tukufu ya Wakristo wenye misimamo mikali Marekani.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, wanaharakati laki tatu Waislamu na Wakristo katika mtandao wa Facebook tayari wameshatangaza kupinga kuchomwa moto Qurani huko Marekani.
Mbali na wanaharakati Waislamu kupinga kitendo cha kuchomwa Qurani, vile vile kuna kundi lijulikanalo kama, "Wakristo dhidi ya Kuchomwa Qurani" ambao wameanzisha ukurasa wao katika Facebook.
653401
captcha