IQNA

Kundi la Kikristo la kimataifa lalaani dharau dhidi ya Uislamu nchini Austria

12:45 - September 18, 2010
Habari ID: 1995908
Kundi la Kikristo la kimataifa la Pax Christi linalofungamana na Kanisa Katoliki limetoa taarifa likilaani kuanza wimbi jipya la mashambulio dhidi ya Uislamu nchini Austria.
Huku likiaashiria kuzinduliwa mchezo ulio dhidi ya Uislamu nchini Austria katika kukaribia kufanyika uchaguzi wa kieneo nchini humo, kundi hilo linalofuatilia masuala ya amani limelaani kitendo hicho na kusema kuwa badala ya kupigwa marufuku ujenzi wa minara na misikiti nchini Austria, majengo hayo ya ibada yanapaswa kuongezwa nchini.
Limesema Waislamu wanahitajia misikiti kwa ajili ya kutekeleza ibada zao na kwamba iwapo jambo hilo litaruhusiwa, basi Waislamu watahisi zaidi kuwa sehemu ya jamii ya nchi hiyo.
Taarifa hiyo imesema katika sehemu nyingine kwamba, demokrasia ya Magharibi pia inajumuisha uhuru wa kuabudu na kwamba maana ye neno hilo katika jamii haipaswi kubanwa. 656647
captcha