IQNA

Mradi wa kuanzisha Bustani ya Itikadi nchini Uturuki

17:12 - September 21, 2010
Habari ID: 1998854
Mradi wa kujenga Bustani ya Itikadi ulianza kutekelezwa siku ya Jumatatu tarehe 20 katika mji wa Mardin nchini Uturuki. Mradi huo unaotekelezwa kwa ushirikiano wa Wizara ya Utamaduni na Utalii ya Uturuki na ofisi ya meya wa Mardin utawawezesha Waislamu na Wakristo kukutana na kujadiliana huko kuhusiana na masuala ya itikadi zao baada ya kutekeleza ibada zao kwenye misikiti na makanisani.
Bustani hiyo inajengwa kati ya msikiti wa Zeinul Abedeen (as) na kanisa la Ya'qub (as) na itakuwa ikitumiwa kwa pamoja na wafausi wa dini mbili hizo.
Waislamu na Wakristo wakaazi wa mkoa huo wamekaribisha mradi huo na kusema kuwa wako tayari kuchangia kila hatua ili kuufanikisha.
Ni vyema kuashiria hapa kuwa mkoa huo umekuwa ukiwakaribisha wafuasi wa dini mbalimbali katika kipindi chote cha historia na kwa msingi huo wakazi wake ni wa tamaduni na staarabu tofauti. Jambo hilo limeimarisha mazungumzo kati ya dini mbalimbali na kunyanyua utamaduni wa kuishi pamoja kwa amani watu walio na utamaduni tofauti. 659665
captcha