Makumbusho hayo yataanza saa kumi na moja alasiri na kuendelea kwa muda wa masaa mawili katika kituo hicho. Katika makumbusho hayo, Hujjatul Islam wal Muslimeen Ahmad Huneif, mwanazuoni raia wa Canada ambaye alipata mafunzo yake ya kidini katika Chuo cha Kidini cha Qum nchini Iran atazungumzia maisha na sifa za Imam huyo wa sita wa madhebu ya Shia.
Makumbusho hayo ambayo yatahudhuriwa na idadi kubwa ya Waislamu wanaoishi nchini Uingereza, yatamalizika kwa kuswaliwa swala ya jamaa ya Maghrib. 660450