IQNA

Fikra za kifiqhi za Allamah Fadhlullah kujadiliwa huko Qatif

15:24 - September 25, 2010
Habari ID: 2000920
Mitazamo na fikra za kifiqhi za Allamah Sayyid Muhammad Hussein Fadhlullah zitajadiliwa katika kongamano litakalofanyika tarehe 29 Septemba katika Husseiniya ya al Mubarak katika mji wa Qatif mashariki mwa Saudi Arabia.
Kongamano hilo litakalofanyika chini ya anwani ya 'Faqihi Mwanadamu' litachunguza fikra za kifiqhi za marehemu Ayatullah Fadhlullah.
Huseiniya ya al Mubarak ya Qatif imetangaza kwamba kongamano hilo litahudhuriwa na maulama na wanafikra wa Kiislamu wa madhehebu ya Shia.
Taarifa hiyo imesema kuwa maulama na wanazuoni watachambua na kuweka wazi mitazamo ya mwanachuo huyo wa kidini katika kongamano hilo. 661845

captcha