IQNA

Masomo ya msingi ya tajwidi na tartili ya Qur'ani kutolewa Doha

16:18 - October 02, 2010
Habari ID: 2005587
Kitengo cha masuala ya dini na vijana cha Kituo cha Vijana cha Doha mji mkuu wa Qatar kinatayarisha masomo ya msingi ya kinadharia na kivitendo ya elimu ya tajwidi na tartili ya Qur'ani Tukufu.
Masomo hayo ambayo yataanza kesho Jumapili yatatolewa na mwalimu mashuhuri wa elimu ya tajwidi wa Qatar Usama al Agha kwa mujibu wa riwaya ya Hafs kutoka kwa Asim.
Usama al Agha amesema masomo hayo ni muhtasari wa taaluma ya Qur'ani kutoka kwenye vitabu vya fani hiyo. Ameongeza kuwa masomo hayo ni fursa nzuri kwa wale wanaotaka kutambua misingi ya elimu ya tajwidi na taaluma ya Qur'ani. 666836

captcha