IQNA

Mashia wa Saudi Arabia kuomboleza kifo cha Imam Swadiq (as)

19:10 - October 03, 2010
Habari ID: 2005941
Mashia wanaoishi katika eneo la as-Sharqiyya nchini Saudi Arabia wamepanga kufanya makumbusho ya kifo cha Imam Ja'far Swadiq (as).
Kwa mujibu wa televisheni ya Raswid, maombolezo hayo yataanza leo Jumapili alasiri katika Husseiniyyah ya Batul katika mji wa al-Awaamiyyah.
Sheikh Naji al-Ibadi atazungumza katika maombolezo hayo kuhusiana na maisha na shakhsiya ya Imam Swadiq (as).
Maombolezo mengine kama hayo pia yamepangwa kufanyika katika Husseiniya ya Abul Fadhl al-Abbas (as) katika mji wa Seihat ambapo Said al-Maatiq mmoja wa mahatibu na wahubiri mashuhuri wa Kishia nchini Saudia amepangiwa kuhutubu.
Maombolezo hayo yatatangazwa moja kwa moja kupitia mtandao wa intaneti kwa anwani ifuatayo: www.abolfadlalabss.com. 667241
captcha