Kikao hicho kilianza kwa kusomwa Qur'ani Tukufu na kisha wageni waalikwa walipewa fursa ya kumzungumzia bibi huyo mtukufu na hasa maisha yake ya kidini na pia nafasi yake akiwa mama na mke mwema.
Wanafikra na wasomi mbalimbali wa Kiislamu walishiriki katika kikao hicho na kutoa mitazamo yao tofauti kuhusiana na sifa pamoja na nafasi muhimu aliyokuwa nayo Bibi Fatma katika kueneza Uislamu katika zama zake. Pia walichambua nafasi ya maisha yake ya mtu binafsi, kijamii na kidini.
Mwishoni mwa kikao hicho washiriki walizawadiwa vitabu vinavyozungumzia maisha ya Bibi Fatma (as) vilivyoandikwa na waandishi wanawake. 668064