IQNA

Duru ya 10 ya mashindano ya kuhifadhi Qur'ani kufanyika Canada

22:28 - October 04, 2010
Habari ID: 2006627
Duru ya 10 ya mashindano ya kuhifadhi Qur'ani tukufu itafanyika katika mji wa Vancouver nchini Canada Aprili mwakani.
Mashindano hayo yatafanyika chini ya usimamizi wa Kituo cha Upashaji Habari cha Kiislamu kikishirikiana na taasisi ya al Amin na shule ya Iqra katika mji wa Vancouver kwa shabaha ya kuwahamasisha watu kihifadhi kitabu kitakatifu cha Qur'ani.
Mashindano hayo yatafanyika katika awamu nane tofauti za kuhifadhi juzuu za Qur'ani Tukufu.
Majina ya watu wanaotaka kushiriki kwenye mashindano hayo yataanza kuandikishwa Disemba mwaka huu.
Mashindano ya 9 ya kuhifadhi Qur'ani ya Canada yalifanyika katika awamu mbili tu na washindi wa tatu wa kwanza walitunikiwa zawadi. 668335



captcha