Kwa mujibu wa The Boston Channel, wakuu wa idara ya masomo ya jimbo la Massachusetts wamesema kuwa hatua hiyo ambayo ni ya kwanza kutekelezwa katika jimbo hilo itaanza kutekelezwa rasmi mwaka ujao wa 2011.
Wamesema wamechukua hatua hiyo ili kuheshimu haki za wafuasi wa dini ya Kiislamu wanaoishi katika mji wa Cambridge kama wanavyofanyiwa wafuasi wa dini mbili nyingine kubwa katika mji huo za Wakristo na Mayahudi.
Wameongeza kuwa si haki kuheshimu siku za mapumziko za Wakristo na Mayahudi katika mji huo na wakati huohuo kuwapuuza Waislamu. 673746