IQNA

Mwanafikra mashuhuri wa Kishia wa Saudi Arabia aaga dunia

12:57 - October 14, 2010
Habari ID: 2012668
Swalih Muhammad as-Sultan, mwanafikra mashuhuri wa Kishia wa Saudi Arabia ambaye pia ni mwanzilishi wa kituo cha kidini cha mji wa al-Mubarriz katika mkoa wa al-Ahsaa aliaga dunia siku ya Jumanne.
Mwanafikra huyo alipatwa na mshtuko wa ubongo na kuaga dunia mara tu baada ya kufikishwa katika hospitali moja ya mjini al-Mubarriz. Alizikwa jana Jumatano ya jana. B
aada ya kupata masomo yake ya msingi katika mji huo mwanafikra huyo mashuhuri wa Kiislamu alipata elimu ya juu ya kidini katika miji mitakatifu ya Najaf na Karbalaa.
Swalih Muhammad as-Sultan aliyezaliwa mwaka 1924 alipata masomo yake kutoka kwa walimu mashuhuri wa wakati huo wa Iraq wakiwemo marehemu Seyyid Muhsin Hakim na Sayyid Abul Qassim Khui. 674774
captcha