Umati wa watu wapatao 600 uliswali swala ya Ijumaa katika eneo la magharibi la jumba la Congerss ya Marekani kwa lengo la kulalamikia ubaguzi na hujuma iliyopangwa inayoendeshwa katika baadhi ya miji ya Marekani dhidi ya itikadi za Waislamu.
Wamemtaka Rais Barack Obama aingilie kati mara moja na kuwafanyia uadilifu raia wa Marekani wasiokuwa Wakristo.
Vilevile Waislamu waliokusanyika katika eneo hilo wametaka chuki inayoendeshwa nchini Marekani dhidi ya Uislamu ikomeshwe mara moja. 675759