IQNA

'Grafiki ya Kiislamu' yatunukiwa zawadi maonyesho ya dijitali Tehran

10:07 - October 21, 2010
Habari ID: 2016863
Katika sherehe za kumalizika Maonyesho ya Kimataifa ya Vyombo vya Habari vya Dijitali Tehran, kibanda cha Kenya chenye anuani ya "Grafiki ya Kiislamu' kimepata zawadi ya kibanda bora.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, katika kitengo cha kimataifa cha maonyesho hayo, mtaalamu wa grafiki ya kompyuta, Ali Njoroge kutoka Kenya amepata tunzo kutokana na kazi zake stadi za kisanaa na kiutamaduni.
Katika kitengo cha uuzaji wa programu za kompyuta, Ibrahim Bahadori kutoka Iran amepata tunzo kutokana na kazi zake asili za Kiirani na Kiislamu za kiutamaduni.
Sherehe za kuzawadiwa wataalamu hao zimehudhuriwa na Waziri wa Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu Sayyed Mohammad Husseini na maafisa wengine wa utamaduni.

679256

captcha