IQNA

Kongamano la kimataifa la Mafunzo ya Qur'ani laanza Croatia

14:52 - October 23, 2010
Habari ID: 2017947
Kongamano la Kimataifa la Mafunzo ya Qur'ani Tukufu makhsusi kwa walimu na mahafidhi wa Qur'ani Tukufu wa nchi za Ulaya yameanza katika mji mkuu wa Ctoatia, Zagreb.
Kongamano hilo la kimataifa linasimamiwa na Shirika la Sayansi, Utamaduni na Elimu la Jumuiya ya Nchi za Kiislamu ISESCO likishirikiana na Jumuiya ya Kuhifadhi Qur'ani na Baraza la Kiislamu la Croatia.
Kongamano hilo linafanyika kwa lengo la kuwaenzi mahafidhi wa Qur'ani, kuwaarifisha kwa walimwengu, kupanua elimu na maarifa yao na kadhalika.
Kongamano hilo pia linajadili jinsi ya kutumia teknolojia ya kisasa katika kufunza Qur'ani, mbinu za kuhifadhi Qur'ani na jinsi ya kuboresha mbinu hizo. 680314

captcha