IQNA

Wanasheria wa ulimwengu wa Kiislamu wanakutana leo mjini Jeddah

17:48 - October 24, 2010
Habari ID: 2018836
Wataalamu wa haki za binadamu wa baadhi ya nchi za Kiislamu wanakutana leo katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Nchi za Kiislamu (OIC) mjini Jeddah Saudi Arabia kwa shabaha ya kuchunguza njia za kukomesha mzingiro wa utawala ghasibu wa Israel didi ya wanchi wa Ukanda wa Gaza.
Wataalamu hao wa haki za binadamu wanatoka nchi za Malaysia, Palestina, Senegal na Saudi Arabia na wanachunguza na kubadilishana mawazo kuhusu njia za kukomesha mateso na mzingiro wa Israel dhidi ya raia wa Gaza.
Mkutano huo unasimamiwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu OIC. Timu hiyo ya wanasheria inakusudia kutekeleza maamuzi yaliyochukuliwa mwaka jana na mawaziri wa mambo ya nje wa nchi wanachama katika jumuiya ya OIC.
Wanasheria hao wa Kiislamu pia wanachunguza suala la mashambulizi yaliyofanywa mapema mwaka huu na jeshi la utawala katili wa Israel dhidi ya msafara wa misaada ya kibinadamu kwa wakazi wa Ukanda wa Gaza. 681131
captcha