IQNA

Jumuiya ya Mabunge ya Kiislamu yaonya kuhusu chuki dhidi ya Uislamu

10:21 - October 26, 2010
Habari ID: 2019700
Jumuiya ya Mabunge ya Nchi za Kiislamu duniani imetoa taarifa ikilaani duru za kisiasa na habari zinazoihusisha dini ya Kiislamu na ugaidi.
Kwa mujibu wa gazeti la Imarati la Al Bayan, katika taarifa hiyo iliyotolewa baada ya kumalizika kikao cha kamati ya utendaji ya Jumuiya ya Mabunge ya Nchi za Kiislamu huko Abu Dhabi, nchi za Kiislamu zimelaani vikali aina yoyote ya kuvunjiwa heshima matukufu ya kidini.
Taarifa hiyo imesema kuwa, 'mapambano ya mataifa dhidi ya ukaliaji mabavu wa kigene na jitihada za kupigania uhuru ni mambo ambayo hayawezi kuhusishwa na ugaidi hata kidogo'.
Jumuiya ya Mabunge ya Nchi za Kiislamu imetoa wito kwa jamii ya kimataifa kuchukua hatua za kukabiliana na misimamo ya kidini inayofurutu mipaka na kuimarisha ushirikiano wa wafuasi wa dini mbalimbali duniani.
682265
captcha