Sahar Beida mke wa mwanaharakati huyo amesema kuhusiana na tukio hilo kwamba askari vamizi hao waliingia nyumbani kwao na kumtia nguvuni mumewe na binti yao na kisha kuchoma moto nuskha hizo za Qur'ani.
Amesema askari hao wa Kizayuni walitoa nuskha hizo katika nyumba yao na kisha kizichoma moto nje.
Tunakumbusha hapa kuwa Wazayuni wamekuwa wakikaririkariri kitendo cha kukosea heshima kitabu kitakatifu cha Qur'ani na hivyo kuumiza hisia za mamilioni ya Waislamu ulimwenguni. 682703