IQNA

Dharau mpya ya Wazayuni dhidi ya matukufu ya Kiislamu

14:03 - October 26, 2010
Habari ID: 2020169
Askari vamizi wa Kizayuni jana Jumatatu walifanya dharau nyingine dhidi ya kitabu kitakatifu cha Qur'ani kwa kuchoma moto nuskha mbili za kitabu hicho baada ya kumtia nguvuni mwanaharakati mmoja wa Kipalestina katika kijiji cha Jews huko katika Ufukwe wa Magharibi wa Mto Jordan.
Sahar Beida mke wa mwanaharakati huyo amesema kuhusiana na tukio hilo kwamba askari vamizi hao waliingia nyumbani kwao na kumtia nguvuni mumewe na binti yao na kisha kuchoma moto nuskha hizo za Qur'ani.
Amesema askari hao wa Kizayuni walitoa nuskha hizo katika nyumba yao na kisha kizichoma moto nje.
Tunakumbusha hapa kuwa Wazayuni wamekuwa wakikaririkariri kitendo cha kukosea heshima kitabu kitakatifu cha Qur'ani na hivyo kuumiza hisia za mamilioni ya Waislamu ulimwenguni. 682703
captcha