IQNA

Nchi 55 katika maonyesho ya vyombo vya habari Iran

12:04 - October 28, 2010
Habari ID: 2021114
Wawakilishi wa vyombo vya habari vya nchi 55 wanashiriki katika maonyesho ya 17 ya vyombo vya habari mjini Tehran.
Kati ya nchi zinazoshiriki ni Kenya, Iraq, Tajikistan, Uturuki, Argentina, China, Syria, Ufaransa na Palestina. Nchi zingine zinazoshirikia ni Tanzania, Uingereza, Albania, Belarus, India, Croatia, Misri, Lebanon, Korea Kusini, Yemen, Qatar, Libya, Georgia, Kuwait, Kyrgyzstan na Russia.
Nchi zote hizo zina vibanda maalumu vyenye maelezo kuhusu nchi husika.
Kitengo cha kimataifa cha Maonyesho hayo kilianza tarehe 25 Oktoba na kitaendelea hadi Novemba Mosi.
Maonyesho hayo yanafanyika katika Ukumbi wa Sala wa Imam Khomeini (MA) mjini Tehran.
682704
captcha