IQNA

Mashindano ya Qur'ani ya Shirika la Mafuta la Iran yakamilika

17:14 - October 30, 2010
Habari ID: 2022240
Mashidano ya 16 ya Qur'ani Tukufu kwa ajili ya wafanyakazi wa Shirika la Taifa la Mafuta la Iran yelimalizika Ijumaa ya jana katika mji Mtakatifu wa Mash'had Kaskazini Mashariki mwa Iran.
Akizungumza na IQNA, Mkuu wa uhusiano wa umma katika Shirika la Mafuta la Iran amesema mashindano hayo yalikusudia kusambaza utamaduni na mafundisho ya Qur'ani miongoni mwa wafanyakazi wa shirika hilo pamoja na familia zao.
Mashindano hayo yalikuwa na washiriki 4000 ambapo 141 kati yao walifika fainali.
684901

captcha