IQNA

Iran, muhuishaji wa Qur'ani na sayansi ya kitabu hicho

16:05 - October 31, 2010
Habari ID: 2022927
Iran ya Kiislamu ni muhuishaji wa Qur'ani na sayansi ya kitabu hicho na hii ndiyo nduvu iliyotajwa na Mwenyezi Mungu katika aya ya 60 ya suratul Anfal ya Qur'ani Tukufu akisema: "Na waandalieni nguvu mziwezao".
Hayo yamesemwa na Umm Abbas al Namir, mtafiti wa masuala ya Qur'ani wa Saudi Arabia katika mahojiano yake na shirika la habari la IQNA. Ameongeza kuwa Iran ya Kiislamu ambayo ni Ummul Quraa ya ulimwengu wa Kiislamu imeweza kuwapa Waislamu uhai mpya na kueneza mafundisho ya Qur'ani baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Amesema kuwa utamaduni wa Qur'ani wa wananchi wa Iran umetokana na taathira za wafasiri wakubwa wa Qur'ani kama Allama Tabatabai na Imam Khomeini Mwenyezi Mungu awarehemu.
Umm Abbas al Namir ambaye ameshiriki katika Kongamano la Kimataifa la Watafiti wa Kike wa Qur'ani ametunukiwa zawadi ya mlinganiaji bora wa mafundisho ya Qur'ani. 684900

captcha