IQNA

Wafungwa 6000 wahifadhi Qur'ani Iran

18:03 - November 01, 2010
Habari ID: 2023722
Zaidi ya wafungwa elfu sita katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wamehifadhi Qur'an nzima au baadhi ya juzuu kufuatia juhudi za Idara ya Magereza nchini.
Mkuu wa Masuala ya Utamaduni katika Idara ya Magereza ya Iran Hujjatul Islam Tahami amesema, 'mbali na wafungwa, wafanyakazi wa magereza pia wanajitahidi kuihifadhi Qur'ani Tukufu'.
Sheikh Tahami ameyasema hayo katika mji wa Mash'had kaskazini mashariki mwa Iran baada ya kuhutubia warsha ya wahubiri wa kidini katika magereza.
Afisa huyo wa Idara ya Magereza ya Iran amesema hivi karibuni kulifanyika mashindano ya Qur'ani katika mji wa Shiraz ambapo wafungwa 330 walishiriki. Ameongeza kuwa mashindano hayo yalijumuisha kuhifadhi, kusoma na kuitafsiri Qur'ani Tukufu.
685708
captcha